Home

OLAS

HESLB Calendar

May 2013
MTWTFSS
12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031



Headlines

Welcome to HESLB
MAOMBI YA MIKOPO 2013/2014 PDF Print E-mail
Written by Administrator   
Tuesday, 14 May 2013 13:46

MAOMBI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU KWA MWAKA WA MASOMO 2013/2014

 

1.0            Utangulizi

Bodi ya Mikopo inawatangazia wanafunzi wote wanaotarajia kujiunga na Vyuo vya Elimu ya Juu kwa mwaka wa masomo 2013/2014, wanafunzi wanaoendelea na masomo na Umma kwa ujumla, kuwa itaanza kupokea rasmi maombi ya mikopo kuanzia tarehe 1 Mei, 2013.

Maombi ya mikopo yatafanyika kwa njia ya mtandao kwa kupitia anuani ifuatayo: http://olas.heslb.go.tz. Vipeperushi maalum vyenye maelezo ya jinsi ya kuomba kwa njia ya mtandao vinapatikana kwenye Vyuo vya Elimu ya Juu, Ofisi za Elimu za Wilaya, kwa Watoa huduma ya Intaneti, Makao Makuu ya Bodi na kwenye Ofisi za Bodi za Kanda. Maelezo hayo pia yanapatikana kwenye tovuti ya Bodi: www.heslb.go.tz.

Waombaji wapya wanatakiwa kulipa ada ya maombi ya mikopo ya shilingi 30,000/=.  Wanafunzi wote walio katika mwaka wa tano au sita wa masomo wanatakiwa kuendelea kulipa ada ya maombi ya shillingi 10,000/=.  Wanafunzi wanaoendelea na masomo katika mwaka wa pili, tatu na nne ambao walilipa ada ya maombi ya shillingi 30,000 katika miaka ya masomo ya 2009/2010, 2010/2011 na 2011/2012  HAWATAKIWI KULIPA TENA ADA HIYO YA MAOMBI YA MIKOPO.

Sifa za waombaji ni kama zilivyotajwa katika kifungu cha 17 cha Sheria Na. 9 ya mwaka 2004 (CAP 178) ambazo ni:

(i)               Kuwa Mtanzania,

(ii)            Kudahiliwa katika chuo cha elimu ya juu,

(iii)         Kutokuwa na njia nyingine za kugharamia elimu ya juu

(iv)          Kufaulu mitihani ya mwaka uliotangulia (kwa waombaji wanaoendelea na masomo)

(v)             Kuwa mhitaji

Aidha, mwongozo na masharti ya utoaji mikopo kwa mwaka wa masomo 2013/2014 utapatikana kwenye Vyuo vya Elimu ya Juu na pia kwenye tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz) baada ya kuridhiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.

2.0            Hitimisho

Bodi inasisitiza kwamba waombaji wa mikopo wazingatie muda uliopangwa na pia kufuata kwa umakini taratibu zote zilizoanishwa katika uombaji wa mikopo.  Kumbuka hakutakuwa na muda wa ziada baada ya muda uliopangwa kupita.

Mwisho wa kupokea maombi ya mikopo ni tarehe 30 Juni, 2013.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mtendaji

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu

Last Updated on Tuesday, 14 May 2013 14:10
 

Who's Online

We have 58 guests online

Quote of the Day

Be Responsible; repay your higher education loan.


Visitors Counter

mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday58
mod_vvisit_counterYesterday0
mod_vvisit_counterThis week58
mod_vvisit_counterLast week0
mod_vvisit_counterThis month58
mod_vvisit_counterLast month0
mod_vvisit_counterAll days1430792

We have: 50 guests, 8 bots online
Your IP: 107.22.127.92
 , 
Today: May 19, 2013
Higher Education Students' Loans Board