Frequently Asked Questions About Loans

HESLB loan application and allocation

Popular Questions


Zipi ni sifa kuu za kupata mkopo wa elimu ya juu?
Mkopo wa elimu ya juu unaombwaje?
Ni nyaraka gani muhimu zinatakiwa wakati wa kuomba mkopo?
Iwapo mwanafunzi/Mwombaji wa mkopo hajaridhika na kiwango cha mkopo alichopatiwa au hajapangiwa mkopo anatakiwa kufanya nini?

General Questions


Mambo gani muhimu yanapaswa kuzingatiwa wakati wa kuomba mkopo?
  • Hakikisha umesaini fomu ya maombi ya mkopo
  • Hakikisha mdhamini wako amesaini fomu yako katika eneo lake
  • Hakikisha fomu yako imesainiwa na kugongwa mihuri na Serikali ya Mtaa au Kijiji chako
  • Hakikisha fomu yako imesainiwa na mwanasheria au hakimu kuthibitisha taarifa zako na za mdhamini wako
Mkopo unatolewa kwenye vipengele (Loanable Items) vipi?
  • Chakula na malazi
  • Ada ya mafunzo
  • Vitabu na viandikwa
  • Mahitaji maalumu ya kitivo
  • Utafiti
  • Mafunzo kwa vitendo
Nifanye nini ikiwa na nina swali kuhusu mkopo wa Elimu ya Juu?
  • Taarifa zote kuhusu mikopo ya elimu ya juu hupatikana kupitia tovuti ya Bodi ya Mikopo
  • Kwa wanafunzi waliopo vyuoni, kila chuo kina afisa anayesimamia masuala ya mikopo. Ulizia ofisi yake na atakuhudumia
Wajibu wa mwanafunzi mwenye mkopo akiwa chuoni ni upi?
  • Kuwasilisha taarifa zake kwa afisa mikopo (Namba ya usajili na taarifa za benki)
  • Kusaini malipo yanayotumwa chuoni kwake ndani ya muda uliopangwa
  • Kutoa taarifa kwa afisa mikopo wa chuo chake mapema, kama kuna tatizo lolote linalohusiana na mkopo wake
  • Kutembelea tovuti ya HESLB ili kupata taarifa mbalimbali za mikopo ya elimu ya juu