Higher Education Students' Loans Board
BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
MASWALI YAULIZWAYO MARA KWA MARA KUHUSU UREJESHAJI WA MIKOPO ELIMU YA JUU Swali: Mwajiri anapaswa kufanya nini baada ya kuajiri wahitimu wapya? Swali: Nini kitafuata baada ya kuwasilisha HESLB orodha ya wahitimu walioajiriwa? Jibu: Baada ya kupokea orodha ya waajiriwa kutoka kwa mwajiri, Bodi itabainisha wafanyakazi walionufaika na mikopo ya elimu ya juu. Baada ya hapo, mwajiri atapaswa kuhakikisha kuwa makato ya kila mwezi kutoka kwenye mishahara ya wadaiwa wa mikopo yanawasilishwa Bodi ndani ya siku kumi na tano (15) baada ya tarehe ya kila mwisho wa mwezi.
Swali: Nini kitatokea endapo mwajiri ataacha kukata mshahara wa mfanyakazi baada ya kuelezwa na HESLB kwamba mfanyakazi huyo ni mdaiwa wa mkopo?
Jibu: Iwapo mwajiri atashindwa kukata ama kukata mshahara wa mdaiwa wa mkopo na kushindwa kuwasilisha makato hayo Bodi ndani ya muda uliopangwa, atatozwa asilimia kumi (10%) ya kiasi cha deni lililopaswa kulipwa kwa kila mwezi ambao makato hayatawasilishwa.
Swali: Ni lini mnufaika wa mkopo anapaswa kuanza kurejesha mkopo wake? Jibu: Mkopo huanza kulipwa inapomalizika miezi 24 baada ya kuhitimu masomo ya elimu ya juu au baada ya kusitisha masomo kwa sababu yoyote ile.
Swali: Je, ajira ya mdaiwa wa mkopo ni jambo linalozingatiwa katika urejeshaji wa mikopo? Jibu: Wanufaika wote wa mikopo ya elimu ya juu wanapaswa waanze kurejesha mikopo mara baada ya miezi 24 baada ya kuhitimu. Lengo la muda huu ni kuwawezesha kutumia elimu waliyoipata kujiajiri au kuajiriwa na hivyo kupata kipato.
Swali: Ni asilimia ngapi hutozwa kama tozo la kutunza Thamani ya fedha kwa kila mdaiwa wa mkopo? Jibu: Madeni yote ya mikopo hutozwa asilimia sita (6%) kama tozo la kutunza Thamani ya Fedha (Value Rention Fee) kwa mwaka.
Lengo la tozo hii ni kutunza thamani ya fedha dhidi ya mfumuko wa bei ili mkopo uwe na thamani sawa wakati utakapotolewa kwa mwanafunzi mwingine mwenye uhitaji katika siku zijazo.
Swali: Ni hatua zipi za kisheria zitachukuliwa kwa wadaiwa ambao hawatarejesha mikopo yao? Jibu: Mdaiwa yeyote ambaye, bila sababu za msingi atashindwa kulipa mkopo atachukuliwa hatua za kisheria. Aidha, mambo yafuatayo yatafanyika:
Swali: Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kampuni zingine binafsi za ukaguzi wana wajibu gani katika urejeshaji wa mikopo? Jibu: Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG) na makampuni mengine binafsi ya Ukaguzi yana majukumu mawili:
Swali: Mnufaika wa mkopo anapaswa kufanya nini ili kulipa deni lake? Jibu: Mara baada ya kuhitimu masomo au kusitisha masomo yake kwa sababu yoyote ile, mnufaika anapaswa aitaarifu Bodi kwa maandishi mahali alipo na hali ya ajira yake na kuanza kurejesha mkopo wake.
Swali: Kwanini HESLB inatoa zawadi kwa waajiri wanaofanya vizuri katika kurejesha mikopo ya waajiriwa wao ambao ni wanufaika? Jibu: HESLB inatoa zawadi kwa waajiri wanaofanya vizuri katika kurejesha mikopo ya waajiriwa wao ambao ni wanufaika ili kutambua mchango wao katika urejeshaji wa mikopo ya elimu ya juu na kujenga mahusiano mazuri na waajiri hao, vilevile inahamasisha waajiri wengine waweze kurejesha mikopo ya wanufaika waliowaajiri
Swali: Je ni waajiri wangapi hadi sasa wameshapata zawadi toka HESLB kwa kufanya vizuri katika urejeshaji wa mikopo? Jibu: Jumla ya waajiri thelathini na saba (37); 15 kutoka Dar es Salaam, 10 kutoka Zanzibar na 12 kutoka kanda ya Arusha wameshapatiwa zawadi kwa kufanya vizuri katika urejeshaji wa mikopo
Swali: Makato huwasilishwaje HESLB? Jibu: Kwa wanufaika waajiriwa, hukatwa asilimia kumi na tano (15%) ya mshahara wa kila mwezi.
Aidha, mnufaika anaweza kulipa kiwango cha chini cha shilingi 100,000/= kila mwezi kupitia Akaunti zifuatazo:
|
MASWALI NA MAJIBU YA UTOAJI MIKOPO
Jibu:
Jibu: Soma mwongozo unaotolewa na Bodi ambao unapatikana katika tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz), kisha, fungua mtandao wa maombi (www.olas.heslb.go.tz) ili ujisajili kwa kutumia namba yako ya mtihani wa kidato cha nne na mwaka uliofanya mtihani huo.
Jibu: Baada ya kujisajili, utapata namba ya kumbukumbu (Control Number) kwenye ‘screen’ ambayo itakuwezesha kufanya malipo ya ada ya maombi ya TZS 30,000/= kwa njia ya benki au simu. Lipa mara moja tu! Kiasi kamili cha TZS 30,000/=
Baada ya kulipa, utapokea ujumbe (sms) wa uthibitisho wa muamala wako utakaokuwezesha kuendelea na hatua inayofuata ya maombi. Jaza hatua kwa hatua.
(mdhamini anaweza kuwa mzazi au mlezi)
wa masomo na sijapata cheti, nitaambatanisha nini?
Jibu: Unatakiwa kujaza namba ya mtihani wa kidato cha sita ambayo itaweza kuhakikiwa na mamlaka husika. Kwa mhitimu wa diploma (Stashahada), unaweza kuambatanisha waraka wa matokeo (transcript).
kwenye ‘Internet Café’? jibu:
mfano ya nje ya nchi, nitawezaje kuendelea kuomba mkopo?
Jibu: Wakati wa kujisajili, unatakiwa kuchagua kipengele cha ‘Non-NECTA students’ na kujaza kama inavyoelekezwa. Mfumo utakupatia namba ya kidato cha nne tofauti na ile uliyojaza ambayo itatambuliwa na mfumo wa Bodi. Namba hii mpya itatokana na taarifa yako ya namba uliyojazwa awali (isiyokuwa ya NECTA).
Jibu: Fomu inafunguka mara tu malipo yanapokamilika. Fomu inapochelewa kidogo kufunguka, mwombaji unashauriwa kutoka (Sign out) na kujaribu kuingia tena (Sign in) katika mtandao ili aweze kuendelea na hatua zinazofuata.
maombi nifanyeje?
Jibu: Unatarajiwa kupokea ujumbe mara tu muamala unapokamilika. Ikiwa hautapata ujumbe ndani ya saa moja (dakika 60) baada ya kufanya malipo, unashauriwa kuwasiliana nasi kwa namba ya simu +255 22 550 7910 au 0736 665 533 au barua pepe info@heslb.go.tz
NMB,TPB, M-pesa, Airtel Money, Tigo-Pesa, T-Pesa itanigomea kulipa na kuendelea?
Jibu: Kwa kuwa kuna njia zaidi ya moja ya kulipia, unashauriwa kutumia njia ya malipo ambayo ni rahisi kwako au inapatikana sehemu uliyopo wakati ukifanya malipo.
Jibu: Utapaswa kubofya kiunganishi cha “Forgotten the Password?” na kisha utapata neno jipya la siri hapo hapo (kwenye screen) mtandaoni.
Jibu: Vyeti vya kuzaliwa na vya vifo vya wazazi lazima vihakikiwe na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) kabla havijapakiwa (uploaded) kwenye mtandao (olams)
Jibu: Ndiyo. Maombi yako yatakuwa hayajakamilika na hivyo kutofikiriwa katika hatua ya upangaji mikopo.
Unapaswa kuhakikisha nyaraka zote (siyo vyeti vya vifo au kuzaliwa tu) zinathibitishwa na mamlaka, taasisi au maafisa waliotajwa katika mwongozo.
Jibu: Unatakiwa kujaza taarifa za mlezi au mtu mwingine anayekulea au kusimamia masuala yako ya Elimu. Ni lazima taarifa za mlezi au msimamizi zithibitishwe na Serikali ya Mtaa unakoishi. Kama mlezi anazo nyaraka rasmi za kukuasili (adoption document) nazo ziambatanishwe.
Jibu: Iwapo uliwahi kuwa mnufaika wa mkopo wa fedha za Serikali, utapaswa kwanza kurejesha mkopo wote au angalau asilimia 25 ya deni lako kabla ya kufikiriwa kupata mkopo mwingine. Deni unalopaswa kulipa utalipata kwenye mtandao (screen) na utatakiwa kulipa kwanza kabla ya kuendelea na maombi ya mkopo mpya.
uthibitisho w aina gani ili kupata mkopo?
Jibu: Mwombaji ambaye ana mahitaji maalum, ni lazima mahitaji na hali yake ithibitishwe na mamlaka husika kama Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) au taasisi za aina hiyo. Taarifa za aina hii zitapekuliwa kuthibitishwa uhalisia na ukweli wake.
masomo, natakiwa kuomba tena mkopo mwaka huu?
Jibu: Unaruhusiwa kuomba upya mkopo mwaka huu. Maombi yako yatapimwa kwa mwongozo na vigezo vya mwaka huu wa masomo. Unashauriwa usome mwongozo kwa makini na kuuzingatia.
Aidha, kama unasoma mwaka wa pili au wa tatu na kuendelea na una uhitaji wa mkopo, unaruhusiwa kuomba kwa kuzingatia vigezo vya mwaka huu.
Simu zinazoonyeshwa kwenye mtandao?
Jibu: Kuna njia mbili za kuwafikia watoa huduma wa kitengo cha usaidizi (Helpdesk) Njia ya kwanza ni kwa simu +255 22 550 7910 au 0736 665 533 na nyingine ni kwa barua pepe info@heslb.go.tz.
Unashauriwa kuwasilisha taarifa au changamoto husika kwa njia ya barua pepe ili wataalamu waifanyie kazi na kukupigia simu kama itahitajika. Kumbuka kuandika mawasiliano yako ya simu itakayotumika kukupigia.
Jibu: Baada ya kuzi-upload na kukamilisha kujaza fomu ya maombi, mwombaji a-print fomu iliyokamilika na kuituma kwa EMS kwenda kwa:
Mkurugenzi Mtendaji, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, Barabara ya Sam Nujoma – Mwenge S.L.P. 76068 14113 DAR ES SALAAM
Jibu: Baada ya Bodi kupokea, kuhakiki na kuchambua maombi ya mikopo, majina ya Wanafunzi watakaofanikiwa kupangiwa mikopo yatatangazwa kupitia tovuti ya Bodi ya Mikopo (www.heslb.go.tz) kabla ya kufunguliwa kwa vyuo vya elimu ya juu walikodahiliwa Wanafunzi husika.
Jibu:
Mafunzo kwa vitendo
Imetolewa na: Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
|