Higher Education Students' Loans Board

  • Dar es Salaam, Tanzania. P.O.Box 76068

  • General call +255 22 286 4643

  • Monday - Friday8:00am - 5:00pm

News & Events


15
November 2023

HATUA NANE (08) KUJAZA FOMU YA 'SAMIA SCHOLARSHIP' MTANDAONI

1. Ingia kwenye  tovuti (www.heslb.go.tz) ili kusoma orodha ya majina ya wanafunzi walengwa wa ‘SAMIA SCHOLARSHIP’ kwa mwaka 2023-2024;

2. Ingia (https://olas.heslb.go.tz) kujaza fomu ya ufadhili;

3. Bofya ‘Apply for Scholarship’;

4. Baada ya kitufe husika kufunguka, chagua ‘SAMIA SCHOLARSHIP’;

5. Jaza namba yako ya mtihani wa Kidato cha IV uliyotumia kuomba udahili (admission) chuoni;

6. Baada ya fomu kufunguka, thibitisha vitu vifuatavyo kwa kubofya ‘confirm & proceed to next step’;

        i. Majina yako,

       ii. Namba za mitihani ya Kidato cha IV na Kidato cha VI,

       iii. Majina ya shule za Sekondari,

       iv. Tahasusi na ufaulu

7. Hakikisha unazingatia yafuatayo;

       i. Pakia picha ya mwombaji yenye vipimo vya 120x150 pixels’, size <1MB format jpg

       ii. ‘Print’ fomu yako kwa kusainisha ukurasa wa pili

       iii. Pakia ukurasa wa pili uliosainiwa kikamilifu kwenye mfumo

8. Kamilisha maombi yako kwa kubofya kitufe ‘submit your application’